MENU

Fun & Interesting

Kwa nini wachache wanatimiza malengo na wengi (92%) wanashindwa | LENZI | Michael Kamukulu

Video Not Working? Fix It Now

Ni takribani watu 4 tu kati ya 10 huweka malengo yao ya mwaka. Na kati yao hao wanne (4) ni asilimia 8% tu huweza kuyafikia malengo hao. Timiza Malengo Yako kwa kuzijua siri, tabia na sifa walizonazo wale wenye kufanikisha malengo yao. Hatua ya muhimu sana ni kuamua kuwa na malengo ya mwaka. Hatua inayofuata ni kuyafanyia kazi hayo malengo. Hata hivyo, kuwa na malengo peke yake haitoshi; bado unaweza kushindwa kuyafikia malengo hayo (kama ilivyo kwa 92%). Fahamu mambo ambayo hufanywa na 8% ya watu wanaoweka malengo yao ya mwaka ambayo 92% walioshindwa hawayafanyi. Mambo hayo ni: 1. Kuwa tayari kubadilika - ili kupata matokeo ya tofauti 2. Kuwa na picha (maono) ya matokeo wanayoyatafuta 3. Kuwa na orodha iliyoandikwa ya malengo yao (kwa wakati) 4. Kugawa malengo kwenye hatua ndogondogo 5. Kukamilisha lengo (hatua) moja kabla ya kuendea na lengo/hatua nyingine 6. Kuomba msaada pale wanapouhitaji 7. kushirikiana na watu wenye mtazamo na malengo yanayoendana na ya kwao Jifunze zaidi na Michael Kamukulu kupitia LENZI @lenzi.michaelkamukulu #malengo #mafanikio #2024 #chaguamwenyeweleo #2023 #lenzi #michaelkamukulu Chapters 00:00 Wachache wanaweka na kufanikisha malengo 00:41 Kwa nini tunaweka malengo? 01:53 Kwa nini wengi hawatimizi malengo 03:06 1. Kuongozwa na picha (maono) ya matokeo 04:49 2. Kuandika Orodha ya Malengo 06:24 3. Kugawa malengo katika hatua 08:01 4. Kukamilisha hatua moja kwa wakati 08:39 5. Kupumzika na Kujitathmini 10:10 6. Kuomba Msaada

Comment