#YAHStoneTown #SalamaNa #PodCast
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL https://bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link https://spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link https://apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link https://bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link https://bit.ly/YahStoneTownAudioMack
YouTube Link http://bit.ly/YoutubeSalamaNa
Ukiwa zako nyumbani umejikalia kwenye sofa unamuangalia Rosaree kwenye TV kwa mara ya kwanza sidhani kama utaweza kugandua macho, pengine ukiwa na watu walokuzidi umri style yake inaweza ikawashtua kiasi na haswa wakiskia anachoimba ni kwa lugha ya Kiswahili ndo kabisa. Ki ufupi binti huyu toka kwenye familia yenye story ambayo kwa ki binadamu si tu yeye pekee amepitia, lakini ni yeye ambaye anafahamika na wengi kati yetu na hii ni nafasi yako na yangu pengine ya kutufanya tuamini kwamba ulichopitia au unachopitia, huko peke yako na pia hayo mambo yana mwisho wake.
Ki kawaida Rosaree sio muongeaji, lakini unapomkuta kwenye ofisi yake ni mtu wa aina nyengine kabisa alojaa ubabe wakati anatema cheche za mashairi yake, swagg za kinyamwezi na kujibeba kwa kipekee haswa, na hiyo ndo tofauti yake na ma rapper wengine hapa Afrika ya mashariki na Afrika kwa ujumla. Ki umbo si mkubwa hata, hata ki umri pia, bado tunaweza kumsamehe kama atakosea wakati anaelekea kwenye safari ya ubora wake. Pia ana haya nyingi, lakini tena, akiwa kwenye zone yake, anakua ‘mnyama’ mwengine kabisa.
Alipokua chini ya Nahreel na Aika muungano wao ulikua mzuri sana, hits kadhaa zake zilitoka kule, so mimi katika mambo nlotaka kujua ni kwanini kila mtu alienda njia yake? Hapa katikati pia kulikua na picha flani ivi ambazo Baraza la Sanaa na Taifa hazikuzipenda na matokeo yake rapper wetu alifungiwa kufanya kazi zozote zinazohusina na mziki kwa muda wa miezi sita, na kuna masuala ya kufanya kazi nje ya nchi bila ya kibali. Mimi na yeye pia tuligusia masuala ya mahusiono. Mahusiano ya Baba yake na Mama yake, na yeye na nduguze wa tumbo moja na wa kufikia na pia muonekano wake.
Rosaree ni mwerevu, mwenye mipango, na anayejiamini, hiyo ndo tofauti yake yeye na waliobaki. Na anajua hilo! 😀
Tafadhali enjoy.
Love,
Salama
Soundtrack Yeah by @MarcoChali https://www.youtube.com/watch?v=Cue1HB4fnLQ
Follow:
Twitter: http://twitter.com/YahStoneTown
Instagram: http://Instagram.com/YahStoneTown
Facebook: http://facebook.com/YahStoneTown